November 22, 2020



LEO Uwanja wa Mkapa kuna vita mpya ya kusaka rekodi ndani ya Uwanja wa Mkapa kwa wanaume 22 ambao watashuka uwanjani kusaka pointi tatu muhimu.

Namungo 2019/20 ilishiriki kwa mara ya kwanza Ligi Kuu Bara ikiwa chini ya Kocha Mkuu, Hitimana Thiery ambaye alifutwa kazi Novemba 18 na mikoba yake ipo chini ya Kocha Mkuu, Hemed Morocco.

 Ikiwa chini ya Thiery, Namungo inayoiwakilisha Tanzania, kwenye Kombe la Shirikisho Afrika ilikutana na Yanga mara mbili na kwenye mechi hizo hakuna ambaye aliibuka na ushindi zaidi ya sare.


Jumla yalipatikana mabao sita, Yanga ikifunga mabao matatu na Namungo pia ilifunga mabao matatu. Walipokuwa wakisaka pointi sita kila mmoja waliambulia pointi mbili.

 

Mchezo uliochezwa Uwanja wa Mkapa, Yanga ililazimisha sare ya kufungana mabao 2-2 na Yanga ilipoibukia Uwanja wa Majaliwa Lindi ililazimisha sare ya kufungana bao 1-1.

 

Rekodi mpya

Leo wanakutana Uwanja wa Mkapa kwa mara nyingine tena kila timu ikiwa inahitaji kuweka rekodi mpya ya kusepa na pointi tatu jumlajumla ndani ya uwanja kwa kuwa hakuna ambaye aliweza kufanya hivyo msimu uliopita. 

Yanga inaingia uwanjani ikiwa na kocha mpya ambaye ni Cedric Kaze ambaye alichukua mikoba ya Zlatko Krmpotic aliyefutwa kazi Oktoba 3 na Namungo pia inainga uwanjani ikiwa chini ya Hemed Morroco ambaye amechukua mikoba ya Thiery.


Kaze kuhusu mchezo huo alisema :-”Ni mchezo mgumu na utakuwa na ushindani mkubwa, ninatambua kwamba ni timu imara na inaleta ushindani ndani ya uwanja ila nimewapa wachezaji wangu mbinu za kupambana,” .

 

Morroco wa Namungo alisema:”Maandalizi na kila kitu kuhusu mchezo kimekamilika ni suala la kusubiri wakati ili kuona namna gani tutakipata kile ambacho tunakitafuta ambacho ni pointi tatu,” .

 

Safu ya ulinzi


Zote zikiwa zimecheza mechi 10, Yanga ni imara kwenye upande wa ulinzi ambapo imeruhusu mabao ya kufungwa matatu huku Namungo ikiwa imefungwa mabao saba.



Safu ya ushambuliaji

Yanga safu yake imefunga mabao 12 na kinara wa ufungaji ni Michael Sarpong mwenye mabao matatu na kwa Namungo wao wamefunga mabao saba na kinara wa utupiaji ni Bigirimana Blaise mwenye mabao manne.

 

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic