December 28, 2020


UONGOZI wa Azam FC umeweka wazi kwamba unahitaji taji la Kombe la Shirikisho ili kurejesha heshima kwenye viunga vya Azam Complex.

Kwa sasa taji hilo lipo mikononi mwa Simba ambayo jana ilikuwa na kibarua mbele ya Majimaji ya Songea, Uwanja wa Mkapa kweye mchezo wa Kombe la Shirikisho.


Simba ilishinda mabao 5-0 kwenye mchezo huo na kuiondoa Majimaji kwenye mashindano ya Kombe la Shirikisho.

Azam FC inayonolewa na Kocha Mkuu, George Lwandamina imetinga hatua ya nne ya mashindano hayo baada ya kushinda mabao 2-0 dhidi ya Magereza ambao ni mabingwa wa Ligi ya Mkoa wa Dar kwenye mchezo wa hatua ya tatu.

Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Azam FC, Abdulkarim Amin, amesema kuwa wanahitaji kufanya vizuri kwenye kila mashindano watakayoshiriki ili kuweza kutwaa mataji.

“Kwenye kila mashindano ambayo tunashiriki malengo yetu ni kushinda, hivyo kazi bado inaendelea na kwenye Kombe la Shirikisho pia tunahitaji kufanya vizuri ili kuweza kutwaa taji kwani hilo linawezekana,” amesema Amin.

2 COMMENTS:

  1. Ubingwa wa VPL mmeushindwa? Azam kombe lenu LA Mapinduzi haya mengine yana wenyewe

    ReplyDelete
  2. Ubingwa wa VPL mmeushindwa? Azam kombe lenu LA Mapinduzi haya mengine yana wenyewe

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic