KIPA namba tatu wa Klabu ya Simba, Salim Juma anatajwa kuwa kwenye hesabu za kutolewa kwa mkopo ndani ya timu hiyo Kwenye dirisha dogo ambalo limefunguliwa Desemba 16.
Juma amekuwa akikosa nafasi kikosi cha kwanza kutokana na ushindani wa namba jambo linalomfanya azidi kujenga ushkaji na nyavu.
Ndani ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2020/21 hajakaa langoni kwenye mechi hata moja ya Simba.
Miongoni mwa timu zinazopewa chapuo ya kumhitaji nyota huyu kwa mkopo ni pamoja na Coastal Union ya Juma Mgunda na Mwadui FC.
Kukosa nafasi kumemfanya ajenge ushkaji na nyavu
ReplyDeleteHao ndiyo aina yetu ya waandishi. Full makanjanja
Delete