December 2, 2020


KIUNGO mkabaji (defensive midfielder) wa kimataifa wa timu ya Taifa ya Uganda Taddeo Lwanga amesaini dili la miaka miwili kuitumia Klabu ya Simba na leo Desemba 2 ametambulishwa rasmi.

Nyota huyo amewahi kuzichezea timu za Express FC, SCV Kampala, Vipers FC na Tanta FC hivyo uzoefu wake na uwezo wake ndani ya uwanja ni sababu ya kupewa dili ndani ya Simba.

Nyota huyo alikuwa kwenye rada za mabosi hao kwa muda mrefu baada ya kiungo wao Gerson Fraga raia wa Brazil kupata majeraha ambayo yatamuweka nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Fraga aliumia kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Biashara United na nafasi yake ilichukuliwa na Said Ndemla ambaye ni mzawa.


 Usajili wa Lwanga unatokana na Shirikisho la Soka Afrika, (Caf) kutoa nafasi za wawakilishi wa mashindano ya kimataifa kusajili wachezaji 10 ili kuongeza nguvu katika mashindano hayo. 


11 COMMENTS:

  1. Usajili mzuri, ukuta ukijengwa fresh Hamna kutetereka hiyo.

    ReplyDelete
  2. Tusunasubiri kuona matendo uwanjani...

    ReplyDelete
  3. Halafu mukashindane na mazembe viungo wa kujipiga ganji tieni pesa hakuna mchezaji humo

    ReplyDelete
  4. Hii post ya mwisho lazima ni ya Utopolo. Mavi yanagonga chupi.

    ReplyDelete
  5. Hamna hiyo ya nguruwe fc ila hapendi kudanganywa kama tunavoambiwa chama milioni 700 wakati hatuna mchezaji wa hata milioni 200 tuache uwongo

    ReplyDelete
  6. Nguruwe fc hapo hamna mchezaji, mbona ametemwa na TANTA FC? kwahiyo hapo kiufupi tu mmepigwa

    ReplyDelete
  7. Hapo sema kweli uongozi umekosea bora ungeanza kuboresha safu ya ulinzi sasa huyu mchezaji ana nn jipya zaidi ya kufunga lile gori la mbali zidi ya gormahia hapo kweli tumepigwa na kwa nn Tanta alicheza mechi 11 tu akatemwa?

    ReplyDelete
  8. 👆👆👆 akili zenu bdo makinda hatuwashangai, mkipevuka akili mtaacha utopolo

    ReplyDelete
  9. Ubora wa timu yake ya taifa unambeba, Uganda wako juu kisoka kuliko sisi. Mnaweza kusema alitemwa kumbe walishindana masilahi. Kuwa kiungo wa timu ya taifa ya Uganda ni dhahiri kiwango chake kizuri pia.

    ReplyDelete
  10. Jamaa yupo vizuri tena Sana.Mbabe wa soka analijua vizuri na mwili unamruhusu.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic