December 1, 2020

 


UONGOZI wa Klabu ya Yanga umethibitisha kuwa mshambuliaji wake mpya Saido Ntibazonkiza atawasili nchini kesho Jumatano usiku.


Nyota huyo ambaye alisajiliwa kwa dili la miaka miwili akiwa mchezaji huru ni tegemeo ndani ya kikosi cha timu ya Taifa ya Burundi akiwa ametupia jumla ya mabao matatu kwenye mechi za kufuzu Afcon.

Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa lengo la kumleta nyota huyo ni kuendeleza kasi ya timu hiyo kufikia malengo yao.

Huu unakuwa ni usajili wa kwanza kukamilika mapema kuelekea dirisha dogo ambalo linatarajiwa kufungulia Desemba 15.

Ataungana na kikosi cha Yanga kilichoweka kambi Kigamboni kikiwa chini ya Kocha Mkuu, Cedric Kaze.

"Kila kitu kipo sawa, mshambuliaji wetu anakuja ndani ya Yanga, kesho Jumatano saa 3:20 usiku atakuwa ashatia timu uwanja wa ndege, hivyo kama ilivyo kawaida yetu mashabiki wa Yanga tujitokeze kwa wingi kumpokea," amesema.

9 COMMENTS:

  1. Haya, nendeni airport mkampokee mwingine, maana wale waliopata mapokezi ya kihistoria wanachofanya uwanjani hakieleweki kabisa

    ReplyDelete
    Replies
    1. Kwani ww kinakuuma nini Yanga wanapofanya mambo yao hata kama hayaleti tija? Au ndio husda ndiyo inayokusumbua? Achana na mambo yasiyokuhusu

      Delete
  2. @Waziri Usipate tabu Itakuwa husda tu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Sawa sawa. Tumuache atapata aibu yeye mwenyewe

      Delete
  3. @Waziri masamehe bure,
    Baadhi ya binadamu ndivyo walivyo, hawapendi wengine wawe na raha

    ReplyDelete
  4. Wanachokifanya hakieleki? Timu inaongoza ligi mlitaka waihamishe Yanga iende wap?

    ReplyDelete
  5. Mtambo wa mabao!!! Ngoja tusubiri mtambo uanze kukoboa nyavu. Raha jipe mwenyewe bwana.

    ReplyDelete
  6. Mikia wanakereka sana kuona sisi tupo mbali nao. Kuwa na magoli mengi bila point za kutosha ni ufala tu😁😁😁😁😁😁😁😁

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic