December 1, 2020




 

KOCHA Mkuu wa Klabu ya Yanga, Cedric Kaze amekiri kuwa wanatarajia kuwafanyia mchujo washambuliaji wa kikosi hicho, ili kupata watakaoweza kuwasaidia na kuwaacha wale watakaoonekana kushindwa kuthibitisha ubora wao.

 

Tangu kuondoka kwa Mkongomani, Heritier Makambo, Yanga imeonekana kuwa na hali ngumu katika safu ya ushambuliaji, ambapo kwa msimu huu pekee mastraika wote wanne wa Yanga wamefanikiwa kufunga mabao matano pekee kati ya 15 yaliyofungwa na timu hiyo.

 

Nyota hao ni pamoja na Michael Sarpong mwenye mabao matatu, Ditram Nchimbi mwenye pasi moja ya bao,Yacouba Songne mwenye bao moja na pasi mbili za mabao.


Kaze amesema: “Ni kweli tatizo la ushambuliaji ndani ya kikosi chetu kwa sasa linaonekana kuingia katika hatua nyingine ya kuwa tatizo sugu.

 

“Ukirejea michezo yetu mitatu iliyopita utagundua kuwa tulikuwa na uwezo wa kushinda kwa mabao mengi tena dakika za mwanzo tu za michezo hiyo lakini kwa bahati mbaya hatukufanya hivyo.

 

“Kwa mfano ndani ya dakika 45 tu za kwanza kwenye mchezo dhidi ya JKT Tanzania tulikuwa tumetengeneza nafasi za wazi tatu ambazo kama tungekuwa makini basi tungepata mabao.

 

“Kutokana na hali hii tumepanga kufanya tathimini ya mwenendo wa washambuliaji wetu, ili kujiridhisha kama tunahitaji kuwapa mbinu nyingine za ziada au tuangalie utaratibu wa kusajili mastraika wengine ambao wataweza kuleta tofauti kwa sababu hatuwezi kuvumilia tunashinda bao moja kwenye kila mchezo,” amesema Kaze.

 

Ushindi huo dhidi ya JKT umeifanya Yanga kufikisha pointi 31 na kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa ligi.

 

7 COMMENTS:

  1. Mlimfukuza Kocha WA kwanza kisa mabao fukuzeni Na huyu.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Acha uzushi na kuteseka..kocha aliyefukuzwa sababu ilikuwa timu kutocheza mpira unaoeleweka na sio sababu ya kutofunga

      Delete
  2. Kaze alusema alihusika katikavusajili wa wachezaji waliosajiliwa na GSM akiwepo Sarpong na Sogne. Sasa vipi tena?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Hata mie nashangaa. Tuliambiwa kocha Kaze alihusika na usajili wa wachezaji wote waliosajiliwa dirisha kubwa, sasa inakuwaje tena??

      Delete
  3. Acha ungo dogo, kazi kuvuruga timu tu😏

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic