January 19, 2021


WAKATI ishu ya mkataba wake ukiibua gumzo kuhusu uhalali wake wa kusaini miaka miwili ama miezi sita, Kocha Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amesema kuwa kazi mpya ya mshambuliaji wake Fiston Abdoul Razak ambaye ni mshambuliaji ni kufunga mabao mengi ili kuipa timu hiyo ushindi.

Kaze amesema kuwa mshambuliaji huyo anamtambua vema na anaamini kwamba anaweza kufanya makubwa ndani ya kikosi hicho.

Razak ambaye ni raia wa Burundi anaungana ndani ya kikosi cha Yanga ambacho yupo mshikaji wake wa kitambo, Saido Ntibanzonkiza ambaye ni raia wa Burundi.

Kaze amesema kuwa:"Kazi kubwa ya Fiston itakuwa ni kwenye kufunga na hilo sina mashaka nalo juu yake kwa sababu ni mchezaji mzuri na anajua kufanya kazi yake kwa umakini.

"Kwa muda tumekuwa tukifanya vizuri ndani ya uwanja ila tatizo lilikuwa kwenye umaliziaji wa nafasi zinazotengenezwa pamoja na namna ya kutengeneza nafasi zenyewe.

"Ujio wake ndani ya kikosi utakuwa ni furaha kwetu na mashabiki kiujumla ni suala la kusubiri na kuona kwa kuwa kila kitu kitakuwa sawa," amesema.

Yanga ipo nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara imecheza jumla ya mechi 18 kibindoni ina pointi 44.

Safu ya ushambuliaji imefunga jumla ya mabao 29 huku ile ya ulinzi ikiwa imeruhusu mabao saba.

Mkataba wa Fiston umekuwa unaleta utata ambapo mchezaji mwenyewe anasema kwamba amesaini dili la miezi sita huku mabosi wa Yanga wakieleza kuwa amesaini dili la miaka miwili.

Nyota huyo amesema kuwa anaamini atakuja kufanya vizuri ndani ya kikosi hicho ambacho kinahitaji kutwaa kombe la Ligi Kuu Bara.

"Nimesaini dili la miezi sita na nina amini kwamba muda nitakaokuwa ndani ya kikosi nitafanya makubwa," .

6 COMMENTS:

  1. Uongozi wa yanga umezoea magumashi magumashi. Yale yale ya morisson halafu mtamroga kijana wa watu. Kama ni miaka miwili lipeni fungu lake, sio mnalipa la miezi sita mnatengeneza document fake ya miaka miwili, mtakuwa kila mwaka mko CAS na FIFA na hakuna mtakachofanikiwa

    ReplyDelete
  2. We ni kuma tu mpumbavu mkubwa ko saleh ni kiongz wa yanga anaewapa wachezaj mikataba

    ReplyDelete
    Replies
    1. sisi tunajuaje kuwa wewe sio ku**.au kwa kuwa wewe unaita wengine..hadi ukafikiria huko ndiyo akili yako iko huko...acha kutumia matusi

      Delete
  3. hahahaha kweli huyo jamaa ni kuma tena ya mnato ambayo haina maji, unapashwa kuelewa kuwa huyu sareh jembe anaandika habari za uongo tu

    ReplyDelete
  4. hahahaha kweli huyo jamaa ni kuma tena ya mnato ambayo haina maji, unapashwa kuelewa kuwa huyu sareh jembe anaandika habari za uongo tu

    ReplyDelete
  5. Kwani mama yako ana nini kama sio hiyo hiyo?

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic