January 26, 2021

 



MSHAMBULIAJI mpya wa klabui ya Yanga, Fiston Abdoul Razak anatarajiwa kutia nchini siku ya Alhamisi ili kujiunga na kambi ya timu hiyo inayojiandaa na michezo ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Fiston ni miongoni mwa wachezaji watatu waliosajiliwa na Yanga katika kipindi cha dirisha dogop ambao wanakuja kukiongezea nguvu kikosi hicho kinachopambana kushinda tajui la Ligi Kuu msimu huu.

Kikosi cha klabu ya Yanga kimeanza rasmi mazoezi ya kujiandaa na michezo ya mzunguko wa pili jana Jumatatu, mazoezi yanayofanyika kwenye kambi yao ya Avic Town, Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Yanga inaongoza msimamo wa Ligi Kuu Bara ambapo imejikusanyia pointi 44 katika michezo 18 waliyocheza mpaka sasa.

 


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic