February 28, 2021


 DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Simba alimbadilishia majukumu beki wake wa kati, Kenedy Juma kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho, Uwanja wa Mkapa kwa kumpa mikoba ya Shomari Kapombe.


Keneddy ambaye aliibuka ndani ya Simba akitokea Singida United ni miongoni mwa mabeki ambao jina lake lipo kwenye orodha ya nyota walioitwa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars.


Juzi wakati African Lyon 0-3 Simba, alipewa mikoba ya kumwaga maji ambapo alionekana akiimudu kazi hiyo huku akitumia nguvu kubwa kuwazuia nyota wa African Sports kupita upande wake.


Gomes amesema kuwa lengo la kufanya mabadiliko kwenye kikosi chake ni kuweza kuwapa nafasi wale ambao hawachezi mara kwa mara pamoja na kuwapa mapumziko wachezaji wengine.

8 COMMENTS:

  1. Ni African Lyon, sio African Sports.

    ReplyDelete
  2. Replies
    1. Inaonesha una makengeza pacha wewe...kila mtu ameona mahali palipoandikwa African Sports halafu wewe unabisha

      Delete
    2. Imeandikwa African Sports, acha ubishi. African Sports ni ile iliyoichapa Yanga juzi juzi, wakati African Lyon ni ile iliyochapwa na Simba juzi hapo

      Delete
  3. Soma uelewe, African sports imetajwa, usibishe kabla ya kujiridhisha

    ReplyDelete
  4. Juzi wakati African Lyon 0-3 Simba, alipewa mikoba ya kumwaga maji ambapo alionekana akiimudu kazi hiyo huku akitumia nguvu kubwa kuwazuia nyota wa African Sports kupita upande wake.

    ReplyDelete
  5. akitumia nguvu kubwa kuwazuia nyota wa African Sports kupita upande wake.

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic