February 28, 2021


 DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba amesema kuwa mchezo wake ujao dhidi ya Al Merrikh utakuwa mgumu tofauti na wengi wanavyofikiria.

Kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika Simba ikiwa ipo kundi A ipo nafasi ya kwanza na ina pointi sita, mechi zake zote mbili imeshinda.

Ilianza kushinda ugenini mbele ya AS Vita 0-1 Simba kisha ikashinda bao 1-0 dhidi ya Al Ahly, Uwanja wa Mkapa.

Mchezo wake unaofuata wa Ligi ya Mabingwa Afrika itakuwa Machi 6, ugenini nchini Sudani, timu hiyo ilikuwa mikononi mwa Gomes kabla ya kuibukia ndani ya Simba Januari 24 kuchukua mikoba ya Sven Vandenbroeck ambaye yupo zake Morocco.

Gomes amesema:"Kuhusu hilo tuna muda mwingi wa kufikiria juu ya mechi ijayo, itakuwa mechi ngumu kwa sababu naijua hiyo timu. Lakini kwa sasa nadhani tunatakiwa kutojipa mawazo sana kuhusiana na mechi hiyo inayokuja.

"Wachezaji wanajua kwamba tunahitaji ushindi ila inahitaji muda na tutapambana ili kupata matokeo chanya ndani ya uwanja, kikubwa sapoti pamoja na umakini kwani kuna kazi kubwa ya kufanya,".

8 COMMENTS:

  1. Yeye anaijua merreck, na merreck wanamjua yeye. Hapo pagumu

    ReplyDelete
  2. Kweli itakuwa ngumu wachezaji wa al merrekh wanafahamu mbinu zake vzr kwahyo inaweza kuwa ngumu kwa simba ukifananisha na alvocheza na al ahly na as vita walijipigia tu

    ReplyDelete
  3. Watakufa tu, simba sc home and away safi tu

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mlisema alipochoze na alhaly. Sasa mmekuwa washabik wa al merekh.

      Delete
  4. Naamini tutapata point 3 au 4 game zote mbili.

    ReplyDelete
  5. Mungu awatangulie tu kwa kila stage

    ReplyDelete
  6. Asalam Aleykum! All games is big game! So we need big saport from all arier cz Simba is not perfect in away.Mingu ibariki Tanzania na uibariki Simba Kwa uwezo wako c ujanja wao

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic