February 8, 2021


 
BAADA ya mapumziko ya muda wa mwezi mzima kwa Ligi Kuu Bara kutokana na timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars kushiriki mashindano ya Chan sasa mzunguko wa pili unarejea.

 

Tumeona kwamba wachezaji ambao walikuwa wanapeperusha bendera ya Tanzania Cameroon wameshinwa kuwatoa kimasomaso Watanzania kwa kusonga mbele hatua ya robo fainali.

 

Imani yangu ni kwamba kuna kitu ambacho wamejifunza na kujua kwamba yale makosa ambayo waliyafanya awali watakuwa imara wakati ujao. Kwenye mpira hakuna namna ya kubadili matokeo hivyo lazima tukubali kwa sasa.

 

Kikubwa ni kukubali kujipanga upya kwa ajili ya wakati ujao ili timu iweze kupata matokeo mazuri na kuendelea kupeperusha bendera ya Tanzania.

 

Licha ya kuondolewa kwenye hatua ya makundi bado vijana walipambana kusaka ushindi ila bahati haikuwa upande wao. Watanzania wanastahili pongezi kwa sapoti yao ambayo wamekuwa wakiitoa kwa Stars.

 

Pia ni fundisho kwa Stars kujua kwamba Tanzania inapenda kuona matokeo ila yote yanawezekana hivyo cha muhimu ni kujipanga na kufanya vizuri wakati ujao.

 

Mzunguko wa pili una ushindani mkubwa hilo lipo wazi hivyo ni muhimu kwa timu kujipanga kufanya vizuri.

Wakati huu wa mzunguko wa pili ni muda wa kukamilisha hesabu kwa kila timu ambayo ilishindwa kuchanga karata zake vyema kutokana na matokeo ambayo iliyapata ndani ya uwanja.

 

Kuanzia zile ambazo zinapambania kusepa na taji la Ligi Kuu Bara zile ambazo zinapambania kubaki ndani ya Ligi Kuu Bara pamoja na zile ambazo zinapambana kupanda Ligi Kuu Bara.

 

Ipo wazi kwamba mwisho wa ligi kuna timu ambazo zitashuka daraja ambapo ikiwa zitashindwa kupambana wakati huu njia yao ipo wazi.

 

Zile za Ligi Daraja la Kwanza ambazo zitapata matokeo mazuri ni wakati wao wa kupanda mpaka kwenye ligi kuu kuendelea kupambana kwa ajili ya maisha mengine ya ushindani.

 

Ni furaha kubwa kwa timu kupanda ligi huku huzuni kubwa ikiwa ni kwa zile ambazo zitashuka ligi kutokana na ushindani ambao huukuta pale wanaposhuka ligi daraja la kwanza.

 

Jambo la msingi ni kila timu kwa sasa kujipanga kwenye mechi zilizobaki ili kupata matokeo chanya ambayo yatawapa pointi tatu zitakazowafanya waweze kubaki ndani ya ligi msimu ujao. 

 

Kuna dakika 90 ndani ya uwanja kwa ajili ya kusaka pointi tatu ambazo ni muhimu kwa kila timu iliyojiwekea malengo  makubwa.

 

Sapoti ambayo timu inapata kutoka kwa mashabiki ni muhimu kulipwa ndani ya uwanja.Kila timu kwa sasa inahitaji kumaliza ligi kwa mafanikio hivyo muda wa mwisho kujipanga ni sasa.

 

Kwa mechi hizi za mwisho pia ni muhimu kwa waamuzi kuendelea kufanya vizuri zaidi kwa kuzingatia sheria za mpira ili kuona kwamba kila timu inashinda bila malalamiko.

 

Wachezaji nao pia ndani ya uwanja kazi yao ni kupambana kusaka ushindi kwa haki bila kuchoka na kufuata sheria za mpira.

 

Ni dakika 90 ambazo zitaamua hatma ya timu ndani ya uwanja pamoja na nafasi ya timu hiyo kwa kuwa pointi zinapatikana kwa ushindi pekee.

 

Juhudi ni muhimu kwa wachezaji na kuzingatia nidhamu nje na ndani ya uwanja hiyo ni njia sahihi kwa timu kuweza kupata matokeo mazuri.

 

Matokeo mazuri ndani ya uwanja pia yanategemea maandalizi mazuri hivyo muda ambao umebaki kwa sasa kabla ya ligi kuendelea utumike vizuri kwa ajili ya maandalizi.

 

Maandalizi mazuri ni silaha ya timu kupata matokeo mazuri kwenye mechi zote kwani hapo ndipo ambapo mwalimu hupata kikosi cha kazi pamoja na kujua namna gani awatumie wachezaji wake.

 

Ligi yetu imezidi kufuatiliwa na wengi jambo ambalo linaamnisha kwamba hatupo nyuma sana kwenye kukua hivyo ni kazi kwa wachezaji pia kulitambua hilo.

 

Ikiwa wataongeza pia juhudi ni rahisi kwao kuweza kutusua na kupata changamoto mpya nje ya Bongo kwani kwa sasa soka imekuwa biashara.

 

Pia mbali na Stars kuna Ligi ya Wanawake nayo pia imekuwa ikendelea na ushindani huku ni mkubwa kwa kila timu kuwa na nia ya kufanya vizuri ndani ya uwanja.

 

Kwa zile ambazo zilikuwa zinakwama kupata matokeo ndani ya mechi zao ambazo wamecheza ni wakati wao wa kujipanga upya na kuanza kwa namna nyingine.

 

Tusisahu pia kuna Ligi ya Wanawake ambayo inaendelea kushika kasi na kila siku ushindani unazidi kukua kwa kasi huku pia.

 

Timu zote nazo zinaingia kwenye mzunguko wa pili ambao ni muda wa kukamilisha ile ngwe ya kwanza iliyoanza na hapa ndipo ambapo bingwa atakwenda kupatikana.

 

Kila la kheri timu zote kwenye maandalizi ya mzunguko wa pili na imani yangu ni kwamba kila kitu kitakwenda sawa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic