KOCHA msaidizi wa klabu ya AS Vita ya nchini Congo, Raoul Shungu amesema kuwa yupo tayari kuisikiliza ofa ya Yanga kama watahitaji aje kuifundisha timu hiyo.
Yanga tayri imemtambulisha kocha Juma Mwambusi kama kocha wa muda wa timu hiyo, huku mchakato wa kumsaka mbadala wa Kaze aliyefutwa kazi Jumapili iliyopita ukiendelea.
Shungu mwenye uraia wa Congo DR, aliwahi kuwa kocha mkuu wa Yanga na kuipa ubingwa wa Ligi Kuu msimu wa mwaka 1998/99 na kuondoka mwaka 2001 na nafasi yake ilichukuliwa na kocha Boniface Mkwasa.
Akizungumzia mpango huo Shungu amesema: “Nimesikia kuwa aliyekuwa kocha mkuu kwa sasa hayupo, sijawasiliana na kiongozi yeyote wa Yanga juu ya kuwa kocha wao lakini kama watakuwa wananihitaji basi nitasikiliza ofa yao ipoje kwangu.
“Nishawahi kuwa kocha wa
Yanga, mpira wa Tanzania naufahamu vizuri na changamoto zake nafurahi niliishi
vizuri wakati nipo Tanzania, muda mwingine napaona kama nyumbani,”
utopolo wanachekesha! kocha msaidizi wa DR Congo Zahera aliwashinda itakuwa huyo msaidizi wa AS Vita
ReplyDeleteSiyo kazi yako,na haikuhusu umbeya wa kiume huo,utelembwe vp?
Deletepovu la nini utopolo...wakati habari yenyewe ni feki...kama Zahera alisema Simba hawana hela ya kumplipa Ibenge...Sasa Yanga ndiyo wana hela ya kumlipa msaidizi wa Ibenge?wasijetembeza bakuri
ReplyDeleteKocha wa Barcelona kachemka pale utopolo sembuse As vital .
ReplyDeleteTeam ishaoza Sasa inatoa harufu tu, ikioza imeoza tu team