March 24, 2021


MBWANA Samatta, nahodha wa kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo wa kesho dhidi ya Equatorial Guinea ambao ni maalumu kwa ajili ya kusaka tiketi ya kufuzu AFCON.

Stars chini ya Kocha Mkuu, Kim Poulsen iliweka kambi nchini Kenya ambapo ilicheza mchezo wa kirafiki mmoja dhidi ya Kenya na ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1.

Samatta amesema:"Tunatambua kwamba tuna kazi kubwa ya kufanya kusaka ushindi kwenye mchezo wetu dhidi ya Equatorial Guinea hilo lipo wazi.

"Ukweli ni kwamba mwalimu ambaye tupo naye anatutambua vizuri kwa kuwa nilifanya naye kazi kwenye timu za vijana na sasa tupo naye kwenye hii timu kubwa ni furaha kwetu.

"Mashabiki wazidi kutuombea dua ili tufanye vizuri nasi tutapambana ili kupata matokeo chanya kila kitu kinawezekana," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic