March 26, 2021


 KOCHA Msaidizi wa Klabu ya AS Vita ya DR Congo, Raoul Shungu amesema kuwa watawahi mapema kuja Tanzania kwa ajili ya mchezo wao wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Simba.

AS Vita inatarajiwa kumenyana na Simba Aprili 3, Uwanja wa Mkapa kwenye mchezo wa makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mchezo wa kwanza walipokutana Congo, Simba ilishinda bao 1-0 ambalo lilifungwa na Chris Mugalu kwa mkwaju wa penalti na kuifanya Simba kusepa na pointi tatu mazima.

Ikiwa Simba ipo nafasi ya kwanza kwenye kundi A na pointi zake 10 inatarajiwa kumenyana na AS Vita iliyo nafasi ya tatu na pointi zake nne.

Kocha huyo amesema:"Mchezo wetu dhidi ya Simba utakuwa na ushindani mkubwa hivyo ili tupate matokeo chanya ni lazima tuwahi kufika eneo la tukio kwa ajili ya kufanya maandalizi ya mwisho.

"Wachezaji wetu wanatambua kwamba haitakuwa kazi rahisi hasa ukizingatia kwamba Simba imekuwa ikipata matokeo chanya kwenye mechi zake inazocheza nyumbani," amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic