March 22, 2021


ZAWADI kubwa ambayo kwa sasa mashabiki wanahitaji kutoka kwa wachezaji wao ni matokeo mazuri kila wakati. Hakuna kingine ambacho mashabiki wanahitaji.

Mwenye kazi ya kuwapa matokeo mazuri ni mchezaji hivyo kazi yake ni lazima iwe kusaka ushindi. Dakika 90 zina maamuzi hayo na ili ifanikiwe ni lazima kuwe na juhudi bila kukata tamaa.

Haijalishi ni mechi ya kirafiki ama ushindani ni jambo moja linatafutwa ushindi baada ya mpira kukamilika masuala ya kusema kwamba bahati mbaya huwa inawaumiza mashabiki.

Kushindwa kupatikana kwa matokeo kwenye mchezo wa kwanza inapaswa iwe somo kwa ajili ya mechi inayofuata. Lakini jambo la msingi kwa wachezaji ni kutambua kwamba zawadi inayohitajika ni ushindi.

Ipo wazi kwamba kwa msimu wa 2020/21 ushindani ni mkubwa na kila timu inajua kwamba inajukumu la kutimiza katika kuyafikia malengo.

Kwa timu ambazo bado hazijawa na mwendo mzuri ni muhimu kwa sasa kufanya kazi ya kurekebisha makosa ambayo wameyafanya.

Kwa timu ambazo matokeo yamekuwa ni ya kusuasua ni muhimu kuongeza nguvu. Ikiwa zitakwama kubadili mwendo matokeo yatakuwa tofauti mwisho wa mzunguko wa pili.

Inawezekana kwa kila timu kuweza kuwa kwenye mabadiliko na kupata matokeo ambayo ni mazuri. Njia pekee ya kufanya hivyo ni kufanya maandalizi mazuri.

Maandalizi yakiwa bora inakuwa rahisi kupata matokeo chanya. Kila mchezaji anapoingia uwanjani huwa anafikiria ushindi ikiwa hajapitia maandalizi mazuri itakuwa ngumu kufikia azma hiyo.

Jambo la msingi ambalo kwa sasa wachezaji wanatakiwa kufanya ni kuongeza akili zaidi kupambania timu zao.

Kwa msimu huu ni timu nne ambazo zitakuwa kwenye nafasi nne za mwisho zitashuka daraja. Pia mbili ambazo zitakuwa kwenye nafasi ya 13 na 14 zitacheza playoff.

Hakuna ujanja wa kukwepa hatua hizi kwa kuwa ligi inaendelea na matokeo lazima yaonekane. Ili kukwepa haya kwa timu ambazo zipo kwenye hatari ya kushuka daraja kazi ni moja kupambana muda wote.

Matokeo mazuri yanahitajika kwa timu ambayo inahitaji kubaki kwenye ligi. Pia kuna vita ya kusaka ubingwa wa ligi pamoja na ile 10 bora.

Hali hii ni nzuri kwa sababu inafanya ushindani unazidi kuongezeka kila wakati uwanjani. Ikiwa kutakuwa na kasi kwenye ligi tutapata wachezaji wengi wazuri ambao watapata nafasi ya kuwa kwenye timu ya taifa.

Habari kubwa kwa timu za Ligi Daraja la Kwanza nao pia ni vita yao ya kuhitaji kushiriki Ligi Kuu Bara. Hapa nao vijana wanapambana kutimiza malengo ambayo wanayo katika timu.

Inawezekana na muda ni sasa wa kuweka mipango kwa umakini. Wakati wa kupanga kwamba kuna kupanda basi ikumbukwe kwamba kuna kushuka pia ikiwa itaboronga.

Kwa kufanya hivyo itakuwa ni rahisi viongozi kuweza kujipanga kwa ajili ya wakati ujao pale ambapo zitashuka daraja. Kikubwa ni kwamba ukipanda unapaswa ujiandae pia kushuka.

Shukrani pia kwa mashabiki ambao wamekuwa wakijitokeza uwanjani kuzipa sapoti timu zao zikiwa kazini. Katika hili pongezi wanastahili.

Kwa sasa ambacho kinatakiwa ni kila shabiki kuwa mstahimilivu pale matokeo yanapokuwa sio zawadi kwa upande wao. Maana yake ni kwamba ikiwa hiyo zawadi haiwahusu basi wapo ambao wanahusika kuichukua.

Utulivu wao utawafanya waiepushie timu yao na adhabu ambazo zimekuwa zikitolewa kutoka Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF).

Pia itawafanya wachezaji kujua kwamba wamekosea kutoa zawadi ya maumivu wanapaswa kutoa zawadi ya furaha kwa mashabiki wakati ujao.

Kushindwa kupata matokeo mechi moja haina maana kwamba hakutakuwa na mechi nyingine hapana. Ni muhimu kujipanga kila wakati kufanya vizuri.

Imani yangu ni kwamba wachezaji wanatambua majukumu yao na mashabiki pia wanajua wanachotakiwa kukifanya wawapo uwanjani.

Kama kila mmoja anajua jukumu lake basi rai yangu kusiwe na ugomvi katika kusaka ushindi hata pale ushindi utakapokosekana baada ya dakika 90.

Maana kwa mechi za hivi karibuni nimekuwa nikishuhudia matukio ambayo si salama kwa afya za wachezaji kutokana na faulo ambazo wanachezeana bila kujali.

Jambo la msingi ni kuona kwamba mzunguko huu wa pili yale makosa ambayo yalikuwa yanafanyika yanapunguzwa ama kuachwa kabisa.

Mzunguko wa pili ushindani wake ni mkubwa kuliko ule wa kwanza. Sababu ni kwamba wakati huu ni muda wa kukamilisha hesabu kwa timu zote.

Rai yangu kwa wachezaji kuwa walinzi wa wengine ndani ya uwanja na kujali afya za wenzao ili wawe salama mpaka pale mpira utakapokamilika.

 

 

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic