April 28, 2021

 


BREAKING: BEKI wa kushoto wa Klabu ya Simba, inayonolewa na Kocha Mkuu, Didier Gomes, Mohamed Hussein,  ameongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia timu hiyo.




Mkataba wa Mohamed ulikuwa umebakiza miezi miwili hivyo wameboresha mkataba huo wa beki huyo mwenye mabao mawili ndani ya Ligi Kuu Bara.

Jina lake lilikuwa linatajwa kuwa kwenye rada za timu kubwa Afrika ikiwa ni pamoja na Kaizer Chiefs ambayo ilikuwa inahitaji saini yake.

Pia ilikuwa inatajwa kuwa mabosi wa Yanga nao walikuwa kwenye hesabu za kuipata saini ya beki huyo mzawa ambaye ni chaguo la kwanza la Gomes.

Habari zimeeleza kuwa mkataba wake umeboreshwa na kuwa ghali kwa wazawa ambapo mshahara wake unatajwa kuwa ni milioni 10 kwa mwezi na umegharimu milioni 100 kwa ajili ya maboresho yake.

Licha ya kwamba mabsi wa Simba hawakuwa tayari kuzungumzia juu ya muda ambao beki huyo ameongeza inaelezwa kuwa ameongeza dili la miaka miwili.

6 COMMENTS:

  1. Kelele za mtaani zimesaidia mtu kupata fedha yake

    ReplyDelete
  2. Meneja wake atakuwa aliishiwa hela, akaamua kupiga biti ili apate za kumuweka mjini

    ReplyDelete
  3. Haya hilo limeisha anzeni jingine. Muhimu timu zijiandae na kipute cha tarehe 8

    ReplyDelete
  4. Mtateseka ns kuweweseka sana Utopolo. Bado mazuri yanakuja.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mawakala wanawajulia namna ya kuwapiga kwa kutumia jina la Yanga. Hongera zao.

      Delete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic