April 16, 2021



BAADA ya kutoonekana kwenye michezo ya

Ligi ya Mabingwa Afrika, wachezaji wa Simba

waliosajiliwa kwa ajili ya michuano hiyo, Junior

Lokosa raia wa Nigeria na Mzimbabwe Peter

Muduha, klabu hiyo imefunguka kuwa sababu

ya kuachana nao ni Kocha Mkuu, Didier Gomes

kutofurahishwa na viwango vyao.

 

Lokosa ambaye yeye ni mshambuliaji

alisajiliwa na Simba akitokea Esperance ya

Tunisia huku beki kisiki, Peter Muduha akitokea

Highlanders FC ya Zimbabwe.

 

Wachezaji hao walisajiliwa Januari, mwaka huu

kwa ajili ya michuano ya kimataifa ambapo

mpaka sasa Simba imefuzu kuingia hatua ya

robo fainali huku wachezaji hao wakiwa

hawajacheza mchezo wowote.

 

“Wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni kwa ajili

ya kucheza michezo ya kimataifa ambao ni

Junior Lokosa na Peter Muduha watavunjiwa mikataba yao hivi karibuni.

 

“Wamekuwa na timu kwa muda mrefu lakini

bado viwango vyao havikuwa bora vya

kumridhisha Kocha Gomes, hivyo huenda

wakasitishiwa mikataba yao mwishoni mwa

msimu huu,” alisema mtoa taarifa huyo.

 

Aidha, kwa upande wa Gomes wakati Simba

ikielekea Sudan kumenyana na Al Merrikh

alisema: “Wachezaji niliowaacha ambao

hawapo kwenye kikosi kinachosafiri akiwemo

Peter Muduha na Lokosa Junior sijafurahishwa

na viwango vyao.”

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic