June 3, 2021

 


UONGOZI wa Yanga umewaomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kuipa sapoti kubwa timu yao katika mchezo wao wa kirafiki unaotarajiwa kuchezwa Juni 6 saa 1:00 usiku.


Mchezo huo utakuwa wa kirafiki ikiwa  ni lengo la Kocha Mkuu,  Nassreddine Nabi kuwaimarisha  wachezaji wake ambapo watamenyana na African Lyon. 


Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli amesema kuwa mashabiki wajitokeze kuipa sapoti timu yao.


"Mashabiki wajitokeze kwa wingi kuipa sapoti timu yao kwani tuna mchezo wa kirafiki dhidi ya African Lyon utachezwa Uwanja wa Azam Complex, " amesema. 


Kiingilio katika mchezo huo mzunguko ni 3,000 na VIP ni 5,000.

3 COMMENTS:

  1. Kishindo chote hicho kumbe mnacheza na African Lyon kama vile mnajipima na timu ya Azam ili washinde tu halafu wajisifu

    ReplyDelete
  2. Ikiwa ndio wanajitaysrisha na mchezo wao na Simba ili kuchukuwa ubingwa basi wsjipime na timu ya kiwango kinachokaribia cha Simba na sio timu iliyodhuks daeaja. Woga sana

    ReplyDelete
  3. Wanaohamasishwa sio mikia kupinda aka paka mweusi!!

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic