July 20, 2021

KOCHA mkuu wa kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania, Kim Poulsen amefunguka kuwa ana matumaini makubwa michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) chini ya miaka 23, yatawaongezea ufanisia zaidi wachezaji wake kuelekea kwenye maandalizi ya michezo ya kusaka tiketi ya kombe la dunia.

Ijumaa ya Julai 16, mwaka huu Poulsen alitangaza kikosi cha wachezaji 20 wanaotarajiwa kuiwakilisha Tanzania katika michuano hiyo mikubwa kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati.

Michuano hiyo kwa mwaka huu tayari imeanza rasmi kutimua vumbi juzi Jumapili ambapo inafanyika nchini Ethiopia.

Akizungumzia mipango yao, kocha Poulsen amesema: “Tuna matumaini makubwa na vijana ambao tumewajumuisha katika kikosi chetu cha U23, hii ni kwa sababu kikosi hiki kina nyota wengi wenye vipaji na uzoefu mkubwa wa mashindano mbalimbali.

“Binafsi naamini tutafanya vizuri kwenye michuano hii, lakini pia tutaitumia kama sehemu ya maandalizi kuelekea kambi yetu ya mwezi Agosti ambayo tutaitumia kwa ajili ya maandalizi ya michezo ya kusaka tiketi ya kushiriki michuano yua kombe la dunia.”


3 COMMENTS:

  1. Unataka tff itoke mbinguni au? Iliyofanikisha kucheza mashindano makubwa ni ipi? Kuweni na shukurani msiwe na akili za kiutopolo

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic