July 25, 2021



IMETHIBITISHWA kuwa uongozi wa Yanga upo kwenye mazungumzo na kiungo wa kimataifa wa Ghana anayecheza soka la kulipwa kwenye Klabu ya Cleopatra inayoshiriki Ligi Kuu ya Misri, Kwame Bonsu ili kumsajili kwa ajili ya msimu ujao wa 2021/22.


Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga

kimelitonya Championi Ijumaa, kuwa tayari

mabosi wa klabu hiyo wamekubali kuliweka jina la kiungo huyo wa Ghana ambaye amesaliwa na

mwaka mmoja tu kwenye mkataba wake wa

Cleopatra, katika listi ya nyota wapya

wanaotarajiwa kusajiliwa kwa ajili ya msimu

ujao wa Ligi Kuu Bara.


“Ni kweli uongozi kwa kupitia kamati yetu ya

usajili umekubaliana na maamuzi ya

kujumuisha jina la kiungo wa Ghana, Kwame

Bonsu kwenye listi ya nyota wapya ambao

wanatarajiwa kusajiliwa kwa msimu ujao.


“Hii ni baada ya kumfuatilia na kugundua kuwa

ni miongoni mwa viungo bora Afrika, lakini pia

ni kiungo mwenye uzoefu mkubwa na

michuano mikubwa, akiwa tayari ameshacheza

kwenye timu kubwa kama Esperance ya Tunisia

na Asante Kotoko ya Ghana.”


Akizungumzia kuhusu usajili wa kiungo huyo,

Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya

Yanga, Thabit Kandoro, alisema: “Kwa sasa

tumesitisha kwa muda kuzungumzia masuala ya

usajili, kwa kuwa bado tuna kibarua cha

mchezo wetu wa fainali ya Kombe la FA dhidi ya

Simba Julai 25, mwaka huu na tutazungumzia

masuala ya usajili baada ya mchezo huo

kukamilika.”


Nyota huyo anakuja kuiimarisha Yanga baada

ya timu hiyo kufanikiwa kusuka safu imara ya

ushambuliaji ambayo inaelezwa itaongozwa na

Wacongo, Heritier Makambo, Fiston Mayele na

Kazadi Kasengu.

Atakuja kufanya kazi na Nasreddine Nabi ambaye ni Kocha Mkuu wa timu hiyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic