September 12, 2021



OFISA Mtendaji Mkuu wa Yanga (CEO), Senzo 
Mazingisa, amesema wamejiandaa kufanya kazi bora na kuijenga Yanga mpya na imara kwa ajili ya kuongeza chachu ya mafanikio zaidi ili kutimiza malengo yao, ikiwemo kutwaa mataji mbalimbali.


Senzo hivi karibuni aliteuliwa na uongozi wa timu hiyo kuwa CEO katika klabu hiyo kwa muda akitoka katika cheo cha mshauri mkuu wa masuala ya mabadiliko ya klabu hiyo.


Akizungumza na Championi Ijumaa, Senzo alisema kuwa wao kama viongozi wamejipanga kufanya kazi kubwa ndani ya Yanga kwa ushirikiano ili kufikia malengo ya timu.


“Sisi kama viongozi tumejiwekea malengo yetu

ambayo mojawapo ni kuifanya Yanga ifikie

katika hatua kubwa ya mafanikio kwa kufanya

kazi kwa ushirikiano ili tufikie hayo malengo.


“Tumejipanga vema kabisa kuhakikisha

tunaifanya kazi hii kwa uzuri kabisa na niseme

tu kuwa sasa tunaenda kufanya kazi ya

kuifikisha katika kilele cha mafanikio ikiwa ni

pamoja na kubeba mataji ya michuano

mbalimbali,” alisema kiongozi huyo.

Leo Yanga ina kibarua cha kusaka ushindi kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa ikiwa ni hatua ya awali dhidi ya Rivers United mchezo unaotarajiwa kuchezwa bila ya mashabiki, Uwanja wa Mkapa.

2 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic