WACHEZAJI wa timu ya Simba ambao hawajaitwa kwenye timu za taifa wameendelea na mazoezi leo Uwanja wa Boko kwa ajili ya kujiweka sawa kwa mechi zao zijazo za ushindani ambapo Simba inawakilisha nchi kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika na pia ina kazi ya kutetea taji la Ligi Kuu Bara.
Didier Gomes leo amewaongoza mastaa waliobaki Tanzania ikiwa ni pamoja na Bernard Morrison, Sadio Kanoute, Inonga pia wale wa ndani ni pamoja na Ibrahim Ajibu, Jonas Mkude.
0 COMMENTS:
Post a Comment