October 7, 2021

DIDIER Gomes, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa wachezaji wake wanazidi kuimarika taratibu na anaamini kwamba kuelekea kwenye mchezo wao wa kimataifa watafanya vizuri.

Simba inatarajiwa kucheza na Klabu ya Jwaneng Galaxy ya Botswana Oktoba 17 ambapo Simba itaanzia ugenini na marudio yanatarajiwa kuwa Oktoba 22.

 Pia ameongeza kuwa hali ya nyota wake Shomari Kapombe inaweza kuwa imara hivi karibuni kwa kuwa wanamuhitaji kwenye mechi ijayo kutokana na ubora wake pamoja na uwezo wa kuongoza kwa sasa anatibu majeraha.

 Kwenye mahojiano ambayo alikuwa akizungumza mbele ya Waanidhi wa Habari Gomes, mashabiki wa Simba wengi walimzonga huku wakihitaji kupiga naye picha.

 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic