WAKATI WA ENZI, WAKIWA NA FURAHA...
Mwanariadha maarufu wa mbio za walemavu, Oscar Pistorius ambaye alishinda
medali ya dhahabu katika Michezo ya Olimpiki iliyofanyika nchini Uingereza,
imebainika alimpiga mpenzi wake risasi nne.
Pamoja na hivyo, tayari kuna taarifa zilizozagaa kwamba ugomvi wao ambao
ulisababisha kifo cha Reeva Steenkamp ambaye ni mwanamitindo
ilitokana na mwanadada huyo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mcheza raga
maarufu, Francois Hougaard.
PISTORIUS KAZINI....
Ingawa wakala wa Hougaard amekanusha lakini taarifa
zinaeleza, Pistorius alishikwa na jazba baada ya kugundua mrembo huyo alikuwa
na uhusiano na mchezaji huyo wa raga ambaye pia anakipiga katika timu ya taifa
ya Afrika Kusini, Springbook.
Taarifa ya polisi wa mji wa Pretoria zimeeleza kuwa
mwanariadha huyo alimpiga mrembo huyo risasi nne, moja kichwani, mkononi,
kwenye hips na mguuni.
ANAYETUHUMIWA KUSABABISHA MFARAKANO HUO AKIWA KAZINI
Mwanadada huyo alijitahidi kukimbia baada ya kupigwa
risasi ya kwenye hips na kujifungia chooni lakini mwanariadha huyo kutokana na
hasira alipiga risasi mlango ukafunguka na kummalizia.
Tayari, Pistorius amepandishwa mahakamani
na uchunguzi zaidi bado unaendelea kuhusiana na tukio hilo lililoshitua wengi
katika nyanja ya michezo.
PISTORIUS MAHAKAMANI JUZI
0 COMMENTS:
Post a Comment