March 23, 2013



 Kiungo nyota wa PSG ya Ufaransa, David Beckham ametoa mpya ya mwaka baada ya kula ‘bonge’ ya mweleka wakati akipiga faulo.

Beckham raia wa England alianguka wakati akionyesha utaalamu wa kupiga mipira ‘iliyokufa’ kwa wachezaji vijana nchini China ambako ana ziara ya kibalozi ya siku tano.

Akiwa ndani ya vazi safi kama mtu anayekwenda ofisini, Beckham alijisahau kwamba hakuwa na ‘njumu’ hivyo kuachia shuti kali nay eye akateleza hadi chini.


Hata hivyo vijana wa timu ya Zall Club walionyesha kutojali hilo la kuanguka kwa Beckham badala yake walifuatilia mpira ulipokuwa umetua.

Yeye Beckham aliinuka mara moja huku akicheka na akaendelea na ratiba zake kama zilivyokuwa zimepangwa.

Ziara ya Beckham nchini humo imekuwa gumzo kwa kuwa amepokelewa kwa makeke na imeonyesha kwamba kweli ni mtu anayekubalika kwa kiasi kikubwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic