March 23, 2013



Mlezi wa Simba, Rahma Al Kharusi leo mchana aliamua kurudisha nguvu zake kwa watoto yatima baada ya kuwatembelea na kula na kunywa na watoto wa kituo cha Umra cha Magomeni Mikumi jijini Dar es Salaam.

Akiwa katika kituo hiyo, Rahma maarufu kama Malkia wa Nyuki, akiwa ameongozana na mwanaye, Fatma walijumuika pamoja na kunywa na kula na watoto hao pamoja na maofisa wa vituo hicho.
 Utamu wa juisi...mwee!
 
Fatma Al Kharusi...
 
Pamoja na kula na kunywa na watoto hao, Malkia wa nyuki alitoa misaada ya vyakula, vinywaji, unga, mafuta kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya kila siku.
Pia Malkia wa nyuki aliahidi kuwafanyia ukarabati nyumba yao iliyo katika eneo la Mbezi Msakuzi, nje ya jiji la Dar es Salaam.

Wakati akiwa kituoni hapo, watoto walionekana kuwa na furaha hasa baada ya kugawiwa jezi nyekundu zenye namba tofauti mgongoni na jina la Malkia.

Watoto hao walionyesha kufurahia ugeni huo kwa kucheza pamoja na mama huyo ikiwa ni pamoja na kuimba nyimbo mbalimbali huku wakionyesa vidole vitano, ‘hata sijui walikuwa wanamaanisha nini’.

Malkia alisema hiyo imekuwa ni kawaida yake kuwatembelea watoto wenye matatizo mara kadhaa kwa lengo la kuwafariji na kuwaonyesha kwamba pamoja na yote, lakini wapo watu wanaowakumbuka.


Lakini pia ni katika kufuata misingi ya dini, kuwasaidia wenye matatizo hata kama utakuwa nacho kitu kidogo tu.

Malkia wa nyuki amekuwa msaada mkubwa kwa Simba ambayo uongozi wake unaonekana kusuasua katika kipindi hiki huku baadhi ya viongozi wakiwa wamejiuzulu.



 Dua...

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic