March 19, 2013



Bocco akichuana na Chuji..

Mshambuliaji nyota wa Azam FC, John Bocco na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo wamekwama kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kwa muda.

Wakati Azam FC imetua nchini leo asubuhi ikitokea nchini Liberia ilipokwenda kuivaa Barrack ya huko, Bocco na wengine kadhaa wamelazimika kusubiri uwanjani hapo.

Kwa mujibu wa uongozi wa Azam FC, Bocco na wenzake watalazimika kusubiri ndege itakayoondoka leo mchana huko kurejea nyumbani.

Azam imelazimika kuwasili nchini kwa mafungu baada ya ratiba hiyo ya Shirika la Ndege la Kenya maarufu kama KQ kuwa na mchanganyiko huo.

Azam FC ambao ni wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya Kombe la Caf, wamewasili nchini na kupokelewa kama mashujaa baada ya kushinda kwa mabao 2-1 ugenini mjini Monrovia.

Hata hivyo, kazi haijaisha dhidi ya Waliberia hao kwani Azam FC italazimika kuulinda ushindi wao katika mechi ya marudiano jijini Dar es Salaam au itakwama.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic