March 19, 2013



Washambuliaji wawili wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wametua nchini na moja kwa moja wamejiunga kambi ya timu ya taifa, Taifa Stars.

Samatta na Ulimwengu wamewasili nchini wakitokea Lubumshashi, DR Congo jana saa 3 usiku na ndege ya Shirika la Ndege la Kenya maarufu kama KQ.

“Kweli wamejiunga na wenzao, tuko nao kambini na kwangu ni kitu kizuri sana kwa kuwa nilikuwa ninawahitaji kwa wakati huu,” alisema  

Stars inatarajia kuivaa Morocco wikiendi hii kuwania kucheza Kombe la Dunia, mechi inayotazamiwa kuwa kali na ya kusisimua.

Tayari Stars ilishaanza kambi jijini Dar es Salaam kujiandaa na mchezo huo ambao ni muhimu kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.

Poulsen amekuwa akiwatumia washambuliaji hao kwa mtindo tofauti, mara nyingi amekuwa akianza na Samatta na Ulimwengu huingia kipindi cha pili.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic