March 15, 2013




Wakazi wa maeneo ya Buseresere na Katoro wameomba michuano ya Amani na Upendo iwe kila mwaka.

Ombi hilo lilitolewa na wanakijiji wa eneo hilo, muda mchache baada ya kumalizika kwa fainali ya michuano hiyo iliyofanyika na kuishia kwa Katoro kuibuka mabingwa kwa kuichapa Buseresere kwa mikwaju ya penalti 5-4.

Ombi hilo lilifikishwa kwa waandaaji ambao ni gazeti la Championi na Mhariri wake Kiongozi, Saleh Ally alisema wanalifanyia kazi na huenda kukawa na jibu zuri.

“Kumekuwa na mafanikio makubwa na tumeona wenzetu wa eneo hili wameipokea michuano hii kwa mikono miwili. Ni gharama kubwa lakini tutalifanyia kazi na imani kubwa itakuwa michuano endelevu,” alisema.


Wakati wa michuano hiyo, mashabiki walikuwa wakijitokeza kwa wingi sana na kuzishangilia timu zao kwa nguvu zote.

Michuano hiyo imeandaliwa ili kurejesha upendo na amani miongozi mwa wakazi wa eneo hilo baada ya vurugu za suala la uchinjaji zilizozababisha mchungaji kuuwawa na muumini mmoja mwislamu kujeruhiwa kwa risasi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic