March 15, 2013




Pamoja na kulazimika kitandani kwa siku mbili kutokana na kusumbuliwa na homa pamoja na mafua makali, Malkia wa Nyuki amesema ataongozana na kikosi cha Simba hadi Kagera na Mwanza.

Rahma Al Kharusi amesema ameamua kuungana na timu hiyo ili kuongeza nguvu katika mechi mbili ambazo ni muhimu sana.

 

“Kweli ninaumwa, nimelazimika kukaa ndani tu hata shughuli zangu nimeshindwa kufanya. Lakini naona nitalazimika kwenda Bukoba kwa kuwa Simba inakwenda na kuna mechi ngumu.

“Mechi hizo mbili ni muhimu sana kwetu, lazima tushinde. Lakini haitakuwa lahisi, hivyo nitaungana na vijana na Wanasimba wote watakaokuwa huko tukapambane.

“Lazima Kagera ni timu nzuri na itakuwa kwao, sisi tutakuwa na timu ya vijana zaidi, lakini walicheza vizuri mechi na Coastal Union ambao pia ni wazuri,” alisema Malkia wa Nyuki.

Baada ya kuivaa Kagera, siku mbili baadaye Simba itarejea jijini Mwanza na kuivaa Toto African iliyo katika wakati mgumu wa kuteremka daraja na lazima itapambana kuokoa 'roho' yake.
Malkia wa Nyuki ndiye amekuwa mhimili mkubwa wa Simba baada ya baadhi ya viongozi wake kuonekana kupoteza dira.

Mwanamama huyo amekuwa tegemeo katika masuala ya ushauri pia kifedha na wanachama na wadau wamekuwa wakitaka apewe sapoti kutokana na anavyojitolea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic