March 15, 2013



 Kipa wa Simba, Juma Kaseja ameonyesha ni mtu mwenye ushirikiano na wachezaji wenzake baada ya kutoa mafunzo ya uhakika kwa makipa makinda wa timu hiyo.

Kaseja ‘raia’ wa Kigoma alifanya hivyo wakati wa mazoezi ya timu hiyo, lakini akaonekana ni kivutio zaidi kwa mashabiki waliojitokeza mazoezini hapo kutokana na ufundishaji wake.

Mara kadhaa, Kaseja alikuwa akiwaelekeza wachezaji hao makinda namna ya kuchutama kwa mipango na kuwa na tahadhari ya wapi mpira utapigwa.

Alitaka wachuchumae, wakashindwa hivyo akalazimika kuwashika makalio ili kuwatafutia balansi. Lakini hapo, maneno yakaanza.



Hata hivyo, Kaseja aliyeonekana kuelewa kinachoendelea, alizidi kuwa siriaz na kuifanya kazi yake kwa ufanisi zaidi.

Kaseja anaamini ndiye kipa bora zaidi wa kipindi hiki na baadhi ya wasaidizi au wanafunzi wake kama Ally Mustapha ‘Barthez’, Deogratius Munishi ‘Dida’ wamekuwa wakijitahidi kumpa upinzani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic