March 19, 2013



Mshambuliaji wa Azam FC, John Bocco amefanikiwa kuripoti kwenye kambi ya timu ya soka ya taifa, Taifa Stars jijini Dar es Salaam.

Bocco amefanikiwa kuripoti katika kambi hiyo baada ya kukwama jijini Nairobi kwa saa kadhaa wakati akirejea nchini kutoka nchini Liberia ambako Azam FC iliichapa Barrack ya huko kwa mabao 2-1 katika mechi ya Kombe la Shirikisho.

Pamoja na Bocco, wachezaji wengine wawili wa Azam FC, Aishi Manula na Mwadini Ally nao waliliripoti pamoja na mshambuliaji huyo. Kabla ya hapo, Mcha Hamis paia wa Azam FC aliliripoti mapema kwa kuwa alipata ndege mapema.

Bocco alichelewa kutokana na Shirika la Ndege la Kenya kuwapangia ndege ambayo ilitakiwa kuingia jijini Dar es Salaam mchana, huku wenzao wengine wakitangulia na ndege iliyotua Dar asubuhi.

Kocha Mkuu wa Stars, Kim Poulsen alisema baada ya wachezaji hao kuripoti, kikosi chake kilikuwa kimekamilika na kilichokuwa kinafuatia ni maandalizi ya kuwavaa Wamorocco.

“Kila kitu safi sasa, familia imekamilika na tunachoendelea nacho ni mazoezi ya pamoja kufikia tunachotaka. Nawashukuru sana vijana wangu kwa kuwahi kambini hata waliochelewa walikuwa na sababu za msingi,” alisema Poulsen raia wa Denmark.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic