March 19, 2013



Tegete akiwa na Nsajigwa...

Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete ameondolewa kwenye ratiba ya mazoezi magumu ili apunguze maumivu ya goti.

Wakati wenzake wakiendelea na mazoezi ya kawaida, Tegete atalazimika kufanya mazoezi ya kawaida na mepesi ili aweze kuendelea na matibabu ya goti.

Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya amesema hali hiyo inatokana na maumivu makali ya goti ambayo yamekuwa yakimsumbua kwa kipindi kirefu kidogo sasa.


“Atakuwa anaendelea na matibabu lakini hatafanya mazoezi magumu kwa kipindi fulani. Baada ya hapo tutakuwa tukiangalia anaendelea vipi ili kujua nini cha kufanya,” alisema Matuzya.

Tegete amekuwa akisumbuliwa na maumivu ya goti ambayo amewai kueleza yanamyima raha uwanjani na kusababisha acheze huku akiwa ana hofu.

Hivi karibuni ameingia katika lawama kubwa pamoja na washambuliaji wengine ya kukosa mabao mfululizo katika mechi zao wanazocheza.

Safu ya ushambuliaji ya Yanga imekuwa ikikosa mabao mfululizo katika mechi zao za Ligi Kuu Bara, hivyo kusababisha timu hiyo inayoongoza ligi kushinda mechi nne mfululizo kwa idadi ya bao moja tu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic