March 15, 2013



Wachezaji wa Simba, jana walikiona cha moto katika mazoezi ya timu hiyo kwenye Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kikhwelo ‘Julio’ alisimamia zoezi la wachezaji hao wakati wanakimbia kwa kasi kubwa kuuzunguka uwanja.

Upande wa pili alikuwepo Kocha Mkuu, Patrick Liewig na muda mwingi Julio ndiye alikuwa anafanya kazi ya kuhamasisha huku akiwataka wachezaji kuongeza kasi.
Mazoezi hayo yalikuwa magumu na Julio alipoulizwa kisa cha yeye kufanya mazoezi hayo, alisema wachezaji wengi wa Tanzania wana uwezo.

“Sasa kama una uwezo halafu hauna pumzi unafikiri unaweza kucheza, haiwezekani. Wachezaji wengi wa Tanzania wana uwezo. Pia mpira uucheze kwa raha, lazima uwe fiti,” alisema Julio.
 Mazoezi hayo yaliendelea kwa saa kadhaa, kabla ya kutoa ruhusa ya kumaliza na baada ya mazungumzo mafupi, wachezaji walipewa ruhusa kurejea makwao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic