March 15, 2013



Mkongwe katika soka ya Tanzania, John Tegete amesema Ligi Kuu Bara inakosa ushindani kutoka katika timu za mikoani kutokana na ukata.

Tegete ambaye ni baba wa mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete amesema ukata katika klabu mbalimbali za mikoani umekuwa ni tatizo kubwa.

“Timu za mikoani zina vipaji sana, lakini tatizo kubwa limekuwa ni ukosefu wa fedha. Ukata unaziua timu za mikoani,” alisema.

“Hata makocha, wazuri ni wengi sana mikoani, lakini wanaangukia katika hali mbaya ya kifedha. Mazingira ya kazi ni magumu sana lakini watu wanajituma sana.

“Nakuhakikishia Simba au Yanga kama wakipewa nafasi ya kuishi maisha ya Toto au timu nyingine za mikoani kwa siku mbili tu, wachezaji wote watakimbia,” alisema.

Mara kadhaa, Tegete amekuwa akilalamika kuhusiana na ukata ingawa timu yake imekuwa ikitoa upinzani mkali kwa timu kubwa kama Yanga, Simba, Mtibwa Sugar na Azam FC.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic