March 14, 2013




Mshambuliaji mwenye kasi wa Simba, Mrisho Ngassa  jana alijikuta katika wakati mgumu katika mazoezi ya timu hiyo.

Simba ilikuwa mazoezini katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam na Ngassa alichelewa kufika takribani dakika 10.

Hali hiyo ilimuudhi Kocha Mfaransa, Patrick Liewig ambaye alimzuia kuanza mazoezi moja kwa moja na kumtaka azungumze na Meneja, Moses Basena ambaye tayari alionekana kuwa amepata maelekezo ya Mfaransa huyo.

Baada ya mazungumzo yaliyochukua takribani dakika sita, Ngassa aliruhusiwa kuungana na wenzake. Ila Wakati huo wengine tayari walikuwa wameanza mazoezi chini ya Liewig na msaidizi wake Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.


Ngassa aliwasili uwanjani hapo harakaharaka akiwa kwenye gari yake aina ya Nissan, alibadili nguo haraka na kutaka kuungana na wenzake, ndipo mzungu ‘alipokomaa’.

Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala alikuwa karibu kabisa akishuhudia Ngassa akibandikwa maswali na Basena kabla ya kuruhusiwa kuingia uwanjani kuanza mazoezi.

Siku chache zilizopita, Liewig alimtimua mazoezini mshambuliaji Felix Sunzu ambaye alitoweka katika timu bila ya kusema lolote kwa siku kadhaa, halafu akarejea na kutaka kuanza tu mazoezi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic