March 18, 2013



Talib akiwa na kikosi chake cha timu ya Oman..
 
Kocha wa zamani wa Simba, Talib Hilal ameendelea kuwanoa makocha na waamuzi mbalimbali wa soka la ufukweni nchini Uganda.

Hilal ambaye aliwahi kuichezea Simba wakati akiwa mwanasoka, ametoa mafunzo ya mchezo huo kwa wiki moja kuanzia Machi 11 hadi 16.

Kocha hiyo imewapatia makocha na waamuzi hao Waganda cheti cha Advance beach soccer kwa kuwa ni ya pili, mwaka 2001 alitoa mafunzo ya kozi ya mchezo huo ngazi ya cheti.


Akizungumza kutoka Kampala, alisema Waganda wamepiga hatua kubwa katika mchezo huo kwa sasa ukilinganisha na Tanzania.

“Wenzetu wamepiga hatua kubwa kwani kwa miaka mitatu sasa wanazo ligi 5 kama Super League, University League, Women League, Youth League na league ya makampuni.

“Wenzetu hawana beach lakini wanatumia mchanga wa Lake Victoria, vipi sisi Tanzania tunazo best beach mpaka leo hatujaanza? Inasikitisha sana. Huu mchezo kwasasa unakuja juu sana unategemea kuwepo kwenye Olympic ya Brazil,” alisema Talib.

Kwa sasa Talib ni kocha wa timu ya taifa ya Oman ya soka la ufukweni na ni kati ya timu zinazofanya vizuri katika mchezo huo duniani.

Tanzania imekuwa ikiendelea kusuasua katika mchezo na inaelezwa kuna kampuni imekabidhiwa kazi hiyo na TFF lakini imekuwa ikiendelea kusuasua.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic