March 23, 2013



Beki wa kati wa Yanga, Ladslaus Mbogo atalazimika kusubiri hadi keshokutwa ili kutolewa nyuzi katika shavu lake baada ya kufanyiwa upasuaji.

Wiki zilizopita, Mbogo maarufu kama Mnyama alifanyiwa upasuaji wa uvimbe katika shavu lake na hali yake imekuwa ikiendelea vizuri.

Daktari wa Yanga, Nassor Matuzya amesema tayari Mbogo ameishatolewa utambi ambao hutumika wakati wa oparesheni.

“Baada ya utambi, litafuatia suala la nyuzi. Jumatatu itafanyika kazi  hiyo na baada ya muda mambo mengine yatafuatia,” alisema Matuzya.

Tayari Mbogo ameruhusiwa kutoka katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam ambako alifanyiwa upasuaji huo.

Uongozi wa Yanga uliamua kuchukua uamuzi wa kumfanya Mbogo upasuaji huo ili kumsaidia, kitu ambacho mchezaji huyo alitoa shukurani zake kama sehemu ya kumuongezea mapenzi zaidi na klabu hiyo.

Mbogo alijiunga na Yanga msimu huu akitokea Toto African ya Mwanza ambako alikuwa mmoja wa mabeki wa kati tegemeo.

Kwa upande wa Yanga, inaonekana analazimika kufanya kazi ya ziada ili kupata namba katika kikosi cha kwanza chenye mabeki wa kati bora kama Kelvin Yondani ‘Cotton’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na Mbuyu Twite.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic