March 19, 2013




Kama inavutiwa na mshambuliaji, Edison Cavani wa Napoli, Man City imeambiwa itoe kitita cha pauni milioni 60 ambayo imetajwa kuwa ni nyingi sana.

Kocha Mkuu wa Man City, Roberto Mancini ndiye amekuwa akivutiwa na mshambuliaji huyo ingawa chaguo lake la kwanza limeelezwa kuwa Radamel falcao wa Atletico Madrid ya Hispania.


Uongozi wa Napoli umeonyesha hauna kipingamizi kabisa na Cavani kutua Man City kama mabingwa hao wa England watakuwa tayari kumwaga fedha hizo walizowatajia.

Rais wa Napoli, Aurelio De Laurentiis amesema mchezaji anaweza kuamua kuondoka au kubaki.

“Inaonekana ni bei kubwa, bado tunamhitaji hapa, uamuzi wa kuondoka uko mikononi mwake. Lakini tunahitaji malipo ya kiwango hicho,” alisema De Laurentiis.

Cavani amekuwa tegemeo la ushambuliaji kwa Napoli lakini inawezekana akakubali kuondoka kwa mambo mawili, kwanza maslahi na pili kubadili mazingira.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic