March 19, 2013




Wadudu nyuki ni hatari sana, hivi karibuni nusura wasababishe mechi ya Ligi Kuu Brazil iahirishwe.

Nyuki hao walivamia uwanja na kuzua tafrani kubwa wakati mechi hiyo ya ligi wiki iliyopita ikiendelea kati ya Ponte Preta dhidi ya Atletico Sorocaba.

Mechi hiyo iliyokuwa ikichezwa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Moisés Lucarelli nusura iahirishwe kwa kuwa nyuki walizidi kuongezeka na kusababisha hofu kubwa kwa watazamanji na hata wachezaji.

Lakini baadaye, nyuki walianza kupungua kwa kiasi kikubwa lakini kundi chache likabaki lililokwenda kuweka kambi kwenye goli moja la uwanja huo.

Kipa akawa hawezi kukaa langoni, hivyo wakalazimika kuitwa wataalamu wa kuuwa nyuki ambao walifika na kufanya kazi hiyo na baada ya hapo mechi hiyo iliyosimama kwa zaidi ya dakika 30 ikaendelea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic