March 19, 2013




Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Mebub Manji, leo jioni ameongoza uzinduzi wa baraza la wadhamini wa klabu hiyo.

Miongozi  mwa wajumbe wa baraza hilo ni pamoja na Balozi Ami Mpungwe, George Mkuchika pamoja na Francis Kifukwe aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Yanga.


Uzinduzi huo ulifanyika kwenye makao makuu ya klabu ya Yanga, mitaa ya Twiga na Jangwani na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo viongozi wengine wa Yanga kama Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga na Katibu, Lawrance Mwalusako na waandishi wa habari.

Yanga imeonekana kupiga hatua zaidi katika kudumisha umoja ndani ya klabu hiyo, kuanzia uwanjani hadi katika masuala ya uongozi.

Mmoja wa wajumbe wa baraza hilo ambaye hakuhudhuria ni Mama Karume ambaye imeelezwa alikuwa safari nje ya nchi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic