March 19, 2013



 Enzi za Moro United ya Ligi Kuu Bara...

Timu ya Moro United iko katika kundi la tatu zilizoshuka daraja kutoka Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kurudi Ligi ya Mkoa msimu ujao wa 2013/2014 baada ya kushika nafasi za mwisho katika ligi hiyo msimu huu 2012/2013 iliyomalizika wikiendi iliyopita.

Moro United iliwahi kuwa moja ya timu vigogo Ligi Kuu Bara wakati ikiwa chini ya mmiliki wake aitwaye Melley Balhabou.

Wachezaji kadhaa nyota walitokea katika timu hiyo akiwemo kipa nyota zaidi nchini, Juma Kaseja ambaye sasa ni nahodha wa Simba, Gaudence Mwaikimba wa Azam FC, Oscar Joshua na Nizar Khalfan wa Yanga. na wengine wengi wanaoendelea kufanya vizuri wakiwa na timu nyingine.

Moro United kutoka kundi B baada ya kumaliza mechi zake ikiwa na pointi tatu. Wakati kutoka kundi C timu iliyoshuka ni Morani ya Manyara iliyomaliza ligi ikiwa na pointi kumi na moja.

Small Kids ya Rukwa imeporomoka kutoka kundi A baada ya kuondolewa kwenye michuano hiyo mapema kwa kushindwa kufika uwanjani kwenye moja ya mechi zake. Kwa mujibu wa kanuni matokeo yote ya mechi ilizocheza yalifutwa.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic