March 18, 2013



Msuva, kushoto akiwa katika mazoezi ya Yanga kujiandaa na mechi mbalimbali za Ligi Kuu Bara

Mashabiki wa Yanga walionyesha kituko pale walipomvamia mshambuliaji wao, Simon Msuva na kuanza kumtishia kuhusiana na ujio wa Mrisho Ngassa aliye Simba.

Mashabiki hao walikuwa wakimueleza Msuva kwamba Ngassa atakapowasili Yanga, basi namba kwake itakuwa ni tatizo na anapoendelea kukosa mabao ndiyo atajiondoa.

 
Msuva alionyesha ustaarabu wa hali ya juu, pamoja na kushambuliwa kwa maneno yakiwemo mengine yanayoudhi, lakini aliendelea kuwajibu vziuri na mwisho akaingia katika basi la timu hiyo.

Kisa cha kumvamia ilikuwa ni kiungo huyo kukosa bao la wazi katika mechi kati ya Yanga dhidi ya Ruvu Shooting.
Pamoja na timu yao kushinda mfululizo na kujichimbia kileleni, mashabiki wa Yanga wamekuwa wakikerwa na kitendo cha ushindi wa bao 1-0 kila mechi.

Yanga imeshinda mechi nne mfululizo kwa idadi hiyo ya bao 1-0, kitu ambacho mashabiki hao wamekuwa wakilalama kupita kiasi.

Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts naye amekuwa akionyesha kukerwa na hali hiyo na hali hiyo ya ushindi finyu unaopatikana.

Ameahidi kwamba atalifanyia kazi suala hilo lakini bado limeng’ang’ania ingawa bado Yanga inazidi kupaa kileleni kwa kuwa inazidi kuchukua pointi tatu katika kila mechi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic