March 16, 2013



1. Tegete akitishia kuondoka na pochi ya Mbogo...

Pamoja na kuwa katika harakati za kufanyiwa upasuaji, beki Ladslaus Mbogo wa Yanga alionekana kuwa makini sana na pochi yake ya kuhifadhia fedha.

 2. Mbogo akisisitiza Tegete arudishe pochi yake chini ya himaya..
Mbogo maarufu kama Mnyama ambaye amefanyiwa upasuaji wa shavu lilikokuwa na uvimbe, hata baada ya upasuaji huo, alihakikisha pochi hiyo ikiwa pembeni chini ya uangalizi wake.


Hali hiyo ilisababisha awe katika wakati mgumu baada ya wachezaji wa Yanga kumtembelea katika hospitali ya Mwananyamala alipolazwa.

Mshambuliaji, Jerry Tegete ndiye alikuwa akihoji kuhusiana na pochi hiyo, alimuuliza Mbogo mara kadhaa kama anaweza akaondoka na pochi hiyo na kuihifadhi au aipeleke kwake.

Pamoja na kukumbushwa kwamba yuko hospitali hivyo hatakuwa na matumizi ya fedha, lakini Mbogo akasisitiza lazima abaki nayo.

Tegete amekuwa akitaniana sana na Mbogo, hivi karibuni beki alichana kiatu cha Tegete baada ya ‘kumuachia’ daruga wakati wakiwa mazoezini.

Mbogo anaendelea vizuri na Kocha Mkuu wa Yanga, Ernie Brandts alikwenda kumtembelea leo ili kumjulia hali.
3. Mbogo akikagua kama kweli Tegete ameweka pochi yake vizuri, Msuva anakufa na kicheko...



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic