March 16, 2013



Mshambuliaji nyota wa Simba, Felix Sunzu ameendelea kuwa katika sakata dhidi ya kocha wake Mfaransa, Patrick Lieiwig.

Siku chache zilizopita, Liewig alimfukuza Sunzu mazoezini kutokana na mchezaji huyo kutoweka bila ya taarifa kwa zaidi ya siku nne, halafu aliporejea akataka kuanza mazoezini.

Liewig amesema Sunzu aendelee kupumzika hadi hapo atakapomuita, hali ambayo imemlazimu mshambuliaji huyo raia wa Zambia kuanza mazoezi kivyake.


Sunzu amesema amekuwa akiendelea na mazoezi gym ili kuendelea kujiweka fiti na iwapo ataitwa mazoezini basi ataungana na wenzake mara moja.

Taarifa zilieleza kuwa sunzu aliondoka kwenda kwao Zambia kimyakimya, lakini yeye amekuwa akisisitiza hakwenda na badala yake alijifungia kwake na kuzima simu.

Sunzu anaonekana kutokuwa na msimu mzuri safari hii, amekaukiwa mabao ya kufunga lakini hata msaada wake unaonekana si mkubwa sana katika klabu hiyo

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic