March 16, 2013




Takribani miaka 10 tokea winga machachari wa zamani wa Yanga
afanye maajabu yake mjini Kampala, Uganda lakini anaendelea kukumbukwa na wadau wengi wa soka.

Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Uganda, Moses Basena amesema Lunyamila anakumbwa Uganda hadi leo.

“Labda kwa watu wa kizazi cha sasa, lakini watu wa umri wangu au chini kidogo, wamekuwa wakiendelea kumkumbuka Lunyamila.

“Nakumbuka kuna wakati hadi magari mfano taxi (daladala) walikuwa wameandika jina lake nyuma. Yote hiyo ilikuwa ni kuonyesha kukubali uwezo wake.
“Lunyamila alikuwa na uwezo mkubwa sana, bado sijaona winga mwenye uwezo wake hapa Tanzania kwa kipindi hiki,” alisema Basena.

Lunyamila aliiongoza Yanga mara mbili mjini Kampala kutwaa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati dhidi ya vigogo SC Villa waliokuwa wanaongozwa na nahodha, Paul Asule.

Lunyamila alikuwa akikabana na Asule aliyekuwa beki wa kulia, shughuli aliyompa ndiyo imesababisha gumzo la winga huyo lisiwe na mwisho.

Lunyamila ambaye ni mchambuzi katika gazeti la Championi ni mmoja wa mawinga bora kabisa waliowahi kutokea katika soka la Afrika Mashariki na Kati.

Lunyamila alikuwa na kasi kubwa wakati akiwa Yanga, lakini baadaye alijiunga na Simba kabla ya kumalizia soka lake Mtibwa Sugar.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic