March 16, 2013



Liewig akiondoka baada ya kuhakikisha Ismail akipanda bajaj...

Kinda Rashid Ismail ameendeleza vituko, safari hii katika mazoezi ya Simba baada ya kuachana na kupanda basi la klabu hiyo aina ya Yutong na badala yake akapanda zake Bajaj.

Ismail ambaye ni mtaratibu, mara tu baada ya mazoezi ya Simba yaliyokuwa yamemalizika katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni jijini Dar es Salaam. Aliamua kuacha basi liondoke.

Wakati Kocha Mkuu, Patrick Liewig akiwa anasubiri usafiri alitaka kujua Ismail ataonoka vipi uwajani hapo.


Mara Bajaj yenye rangi nyekundu iliingia kwa mbwembwe eneo hilo, ikapiga ‘turn’ na kupaki karibu kabisa na Ismail.

Kuona hivyo, Liewig akamuuliza Ismail kama huo ndiyo usafiri aliokuwa anasubiri, alipokubali, kocha huyo alicheka na kutikisa kichwa kisha akaondoka na kusema: “umenichosha kabisa.”

Wakati huo, wachezaji wengine walikuwa wameondoka na magari yao na baadhi wakipanda basi hilo lenye chata za Kilimanjaro lililokuwa linapita mjini na baadaye Kariakoo.

Hivi karibuni, Ismail alihudhuria kuangalia mazoezi ya Yanga mara mbili katika Uwanja wa Bora Kijitonyama  na kuzua gumzo.

Hata hivyo kinda huyo amekuwa akisisitiza alikwenda kuangalia mazoezi katika uwanja huo wa Kijitonyama ambao alichipukia kisoka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic