March 15, 2013




Pamoja na kutoswa na klabu ya Simba, mshambuliaji Danny Mrwanda ameanza kuonyesha makali yake akiwa na timu yake mpya ya Da Nang FC ya Vietnam.

Mrwanda ameanza vizuri na klabu yake hiyo mpya baada ya kufunga bao moja kati ya matatu timu yake iliyopata wakati ikipambana na Kantalan ya Malaysia katika michuano ya Asia Cup.


Da Nang FC ikiwa nyumbani ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 huku Mrwanda aliyejiunga nayo msimu huu akifunga la kwanza.
Timu hizo zitarudiana wiki mbili zijazo, safari hii akina Mrwanda watakuwa ugenini Malaysia.

Mrwanda alitoswa na Simba katika hatua za mwisho baada ya kuonekana kiwango chake si kizuri.

Lakini yeye alisisitiza kuwa alikuwa ameongezeka uzito kwa kuwa baada ya kumaliza mkataba wake na Long Dont Tam hakufanya mazoezi ya kutosha, hata hivyo hawakumsikiliza na kuamua kuachana naye.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic