March 15, 2013




Wakati ina kibarua kigumu ugenini dhidi ya Kagera Sugar, Simba imeamua kuchukua vijana wengi na kwenda kupambana mjini Bukoba.

Simba inaondoka leo Jumamosi na kundi la vijana hao kwenda kuwavaa Kagera Sugar ambao ni wagumu kama ‘nyundo’ wanapokuwa kwao.

Kocha Patrick Liewig amesisitiza anawaamini vijana wake na ana imani watafanya vizuri.

“Nawaamini sana, matokeo ni kitu kinachofuatia. Simba ina mpango wa muda mrefu na sasa kila anayepata nafasi lazima acheze kwa ajili ya timu,” alisema.

Baadhi ya wakongwe walio katika kikosi hicho ni pamoja na Juma Kaseja, Mrisho Ngassa, Amri Kiemba, Said Nassor 'Chollo', pia Kiggi Makasi.

Simba imeondoka bila ya wakongwe kama Felix Sunzu, Abdallah Juma ambao wako kwenye mgogoro na kocha Liewig.

Lakini imewaacha Paul Ngalema na Amir Maftah wanaoelezwa kuwa ni wagonjwa lakini inaelezwa kuna mgogoro kati yao na benchi la ufundi kama ilivyo kwa Mwinyi Kazimoto, Ramadhani Chombo, Haruna Moshi ‘Boban’ na Juma Said Nyosso.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic