March 14, 2013

Ismail (katikati) akiwa na Malkia wa nyuki na Kaseja 

Mshambuliaji kinda wa Simba, Rashid Ismail ambaye alihudhuria mara mbili mazoezi ya Yanga na kuzua gumzo kubwa, ameikana timu hiyo.

Ismail ameendelea kusisitiza alikwenda kuangalia mazoezi akiwa kama mdau wa soka, lakini akasisitiza hakuwahi kuchezea Yanga B kama ambavyo imekuwa ikielezwa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Ismail alisema hakuwahi kuichezea Yanga na timu yake ya kwanza kubwa ni Simba.

“Nimesikia sana taarifa za mimi kucheza Yanga B, inawezekana watu wananichanganya na mtu mwingine. Sijawahi kabisa, ingekuwa ni hivyo wala nisingeficha kwa kuwa si kitu kibaya. Naomba uwaeleze, sikuwahi kucheza Yanga,” alisema Ismail ambaye ni mtaratibu.

Ismail alikuwa katika kikosi cha Simba kilichoundwa na wachezaji chipukizi wengi, ambacho kiliiangamiza Coasta Union iliyokuwa imepania kuichapa Simba.

Kutokea kwake katika mazoezi ya Yanga kwenye Uwanja wa Bora, Kijitonyama jijini Dar es Salaam kumezua gumzo kubwa miongozi mwa wadau wa soka nchini.

Ismaili alihudhuria mazoezi ya Yanga mara mbili, mara ya kwanza mashabiki wa Yanga walionekana kupandwa jazba baada ya kumuona, lakini siku moja baadaye akahudhuria tena na kushuhudia mazoezi hadi mwisho chini ya Kocha, Ernie Brandts.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic